Header Ads

Barnaba Ashindwa Kuvumilia Amjibu Aliyekuwa Mkewe Wa Zamani

Masaa machache baada ya aliyekuwa mke wake ambaye pia ni mzazi mwenziye, kuposti picha akiwa na mpenzi wake wa sasa na kuandika ujumbe unaoelezea sababu za ndoa yao kuvunjika, mwanamuziki wa Bongo Fleva, Barnaba Classic, naye ameandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram ambao umemaanishwa na mashabiki kama amemjibu mkewe.


“Mama aliniambia ukimtukana mwanamke basi umenitukana na mimi, siku zote nawaona kama mama zangu, hongera wanawake wote duniani, salamu zangu juu yenu Jumapili ya leo nawapenda sana, na wale mliopoteza mama zenu fanyeni ibada juu yao waweze punguziwa adhabu ya kifo au kufutiwa kabisa, Bwana Yesu asifiwe sana Jumapili ya Mungu tumpe Mungu Wakristo wenzangu” ameandika Barnaba

No comments

Powered by Blogger.