Header Ads

Mtu Mmoja Nchini Msumbiji Alazimishwa Kuoa Maiti

Dola za Marekani
Mtu mmoja kusini mwa Msumbiji katika mkoa wa Inhambane alilazimika kumlipia mahari mkewe aliyefariki wikendi iliopita kwa Mujibu wa  chombo cha habari cha taifa.

Baada ya mkewe kufariki kutokana na matatizo ya kujifungua ,ndugu zake walimlazimisha mwanaume huyo  kulipa ''Lobolo' (Mahari)', la sivyo hakuna kuzika mwili wa marehemu.

Ndugu zake walimshutumu kijana huyo kwa kushindwa kuafikia majukumu yake ikiwemo kutambulishwa kwa jamaa na ndugu za mwanamke huyo kabla ya janga hilo kutokea.

Ili kuhakikisha kuwa mazishi hayo yanafanyika, kijana huyo alilazimika kumnunulia nguo na viatu mkewe aliyefariki, kisha kukubali kulipa zaidi ya dola 800 na kufunga harusi.

Ndugu mmoja wa  kijana huyo aitwae Irmao do Jovem alielezea kuwa.
''Tulijaribu kuchangisha fedha walizotaka, lakini tuliweza kuchangisha dola 178 pekee.Hivyobasi ilibidi kuweka ahadi ya kulipa fedha zilizosalia siku ya harusi''.

Huku ikiwa familia ya kijana huyo imekubali kulipa,walishutumu tabia ya familia ya mwanamke huyo.

Hatahivyo, ni utamaduni miongoni mwa makabila mengi nchini Mozambique hususan iwapo mwanamume anaamua kuishi na mwanamke bila kufuatilia utamaduni wa kumuoa mwanamke huyo.


No comments

Powered by Blogger.