Header Ads

Ni Marufuku Kuvaa Jezi Ya Barcelona Saudi Arabia Ukikutwa Jela Miaka 15



Kwa Mujibu Wa  mtandao Maarufu wa dailymail.co.uk wa Uingereza, Ni marufuku kuvaa  jezi ya FC Barcelona imefungiwa nchini Saudi Arabia na ukikutwa umevaa unaweza kufungwa.

Jezi ya FC Barcelona yenye nembo ya Qatar Airways imefungiwa kuvaliwa na watu Saudi Arabia na ikitokea umevaa unaweza kupigwa faini ya pound 120,000 ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 300 na kifungo cha miaka 15 jela.

Jezi za Barcelona ambazo zina logo ya Qatar Airways ambao wamekuwa wadhamini wao katika kipindi cha miaka minne iliyopita, Saudi Arabia inaripotiwa kuwa logo ya Qatar Airways ipo nje kisheria au kinyume na taratibu, hivyo ukikutwa utakutana na adhabu ya kifungo.

Habari Njema  ni kwamba FC Barcelona wataanza kuvaa jezi zikiwa na mdhamini wao mpya Rakuten kuanzia msimu ujao wa 2017/18   hivyo mashabiki wa FC Barcelona nchini Saudi Arabia watakuwa na nafasi ya kuvaa jezi za timu yao zenye logo ya Rakuten na sio ya Qatar Airways.


No comments

Powered by Blogger.