Header Ads

MFALME MSWATI WA III AOA MKE WA 14

MFALME Mswati wa Tatu wa Swaziland kwa mara nyingine ameongeza idadi ya wanawake kwa kuoa mwanamke mwingine. Katika kuadhimisha Ngoma ya Umhlanga ambayo hufanyika kila mwaka kwa kumpa mfalme fursa ya kuchagua mwanamke wa kuoa, mfalme huyo hivi karibuni alimchagua Siphele  mwenye umri wa miaka 19 kuwa mkewe wa 14.


Msichana huyo ambaye ni binti wa waziri Jabulile Mashwama katika serikali ya nchi hiyo, alipewa manyoya maalum mekundu ya ndege anayejulikana kama emagwalagwala ambaye huhusishwa na sherehe hiyo maalum ya kifalme. Mswati ambaye ana umri wa miaka 49 huchagua wanawake waliovuka umri wa miaka 19.

Wakiwa kwenye sherehe za mavuno.

Pamoja na talaka kupigwa marufuku katika nchi hiyo ya kifalme, Mfalme Mswati amewahi kuwataliki wake zake watatu. Siphele ambaye ni mhitimu wa Waterford Kamhlaba World University College, alifuatana na Mfalme Mswati alipohudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa hivi karibuni.

Habari hiyo ilifichuliwa na msimamizi wa sherehe za kifalme, Hlangabeza Mdluli, aliyethibitisha kwamba Mswati alikuwa amefuatana na mkewe huyo ambaye kwa umri ndiye mdogo zaidi.

Wake wengine wa Mswati
Wake zake wengine ni pamoja na: Inkhosikati LaMatsebula, Inkhosikati LaMotsa, Inkhosikati LaMbikiza, Inkhosikati LaNgangaza, Inkosikati LaMagwaza (ameachika), Inkhosikati LaHoala (ameachika), Inkhosikati LaMasango, Inkhosikati LaGija (ameachika).

Wengine ni: Inkhosikati Magongo, Inkhosikati LaMahlangu, Inkhosikati LaNtentesa, Inkhosikati LaNkambule, Inkhosikati Ladube na Inkhosikati LaFogiyane. Mfalme King Mswati, anayejulikana pia kama Ngwenyama, yaani simba, anasemekana kuwa na watoto zaidi ya 13 ambao ni pamoja na binti yake mkubwa zaidi aitwaye Sikhanyiso, Sibahle Dlamini, Makhosothando Dlamini, Majaha Dlamini, na Tiyandza Dlamini.

Wengine ni Sakhizwe Dlamini, Saziwangaye Dlamini, Bandzile Dlamini, Lindaninkosi Dlamini, Mcwasho Dlamini, Temtsimba Dlamini na Temaswati Dlamini, among others. Baba yake Mswati, Mfalme Sobhuza wa Pili, alioa wanawake 70. Mswati amekuwa akishutumiwa kwa kujilimbikizia utajiri wakati watu wake wengi ni maskini.
Hivi karibuni, nchi hiyo ndogo ilitumia kiasi cha Dola milioni 2.2 (sawa na Sh. bilioni 5) kwa kununua magari ya anasa aina ya BMW 740i na pikipiki 80. Magari hayo yalikuwa ni kwa ajili ya viongozi wa Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrikca (SADC) waliyoyatumia kwa ajili ya mkutano wa siku mbili.

No comments

Powered by Blogger.